30 Basi Yehova akalitia jiji hilo na mfalme wake pia mkononi mwa Israeli, nao wakalipiga jiji hilo na kila nafsi iliyokuwa ndani yake kwa makali ya upanga. Hawakuacha mtu yeyote aokoke ndani yake. Kwa hiyo wakamtendea mfalme wake kama vile walivyomtendea mfalme wa Yeriko.+
32 Kwa hiyo Yehova akatia Lakishi mkononi mwa Israeli, nao wakaliteka siku ya pili, wakalipiga kwa makali ya upanga na pia kila nafsi iliyokuwa ndani yake,+ kulingana na yote ambayo walikuwa wamelitendea Libna.