20 Hivyo Sauli na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaitwa nje.+ Wakaenda mpaka kwenye pigano, na tazama, upanga wa kila mmoja ulikuwa umeinuka juu ya mtu na mwenzake;+ machafuko yalikuwa makubwa sana.
23 Na wana wa Amoni na Moabu wakasimama kushambulia wakaaji wa eneo lenye milima la Seiri+ ili kuwaangamiza na kuwaharibu; na mara tu walipowamaliza wakaaji wa Seiri, wakasaidiana kuangamizana wao kwa wao.+
2 “Nami nitawachochea Wamisri juu ya Wamisri, nao hakika watapigana kila mmoja na ndugu yake, na kila mmoja na mwenzake, jiji juu ya jiji, ufalme juu ya ufalme.+
21 “ ‘Nami nitaita upanga juu yake kotekote katika eneo langu lote lenye milima,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ ‘Upanga wa kila mmoja utakuwa juu ya ndugu yake.+
13 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba mvurugo kutoka kwa Yehova utaenea katikati yao;+ na kila mmoja wao ataukamata mkono wa mwenzake, na mkono wake utainuka juu ya mkono wa mwenzake.