7 Ndipo Samsoni akamwambia: “Wakinifunga kwa kamba mbichi saba za kano,+ ambazo hazijakaushwa, ndipo nitakuwa dhaifu na kuwa kama mwanadamu wa kawaida.”
13 Kisha Delila akamwambia Samsoni: “Mpaka sasa umenichezea, ukaniambia uwongo.+ Niambie unaweza kufungwa na kitu gani.”+ Ndipo akamwambia: “Ukifuma hii misuko saba ya nywele za kichwa changu kwa uzi wa mtande.”+
15 Mwanamke akamwambia: “Unawezaje kuthubutu kusema, ‘Nakupenda,’+ ingawa moyo wako haupo pamoja nami? Umenichezea mara tatu hizi nawe hujaniambia nguvu zako zinatokana na nini.”+