11 Baadaye Sauli akatuma wajumbe+ kwa nyumba ya Daudi ili wailinde na kumuua asubuhi;+ lakini Mikali mke wake akamwambia Daudi, akisema: “Usipoiponya nafsi yako usiku wa leo, kesho utakuwa mtu aliyeuawa.”
26 Mwishowe Sauli akaja upande huu wa mlima, na Daudi na watu wake wakawa upande mwingine wa mlima huo. Basi Daudi akafanya haraka kuondoka+ kwa sababu ya Sauli; wakati huo wote Sauli na watu wake walikuwa wakimzunguka Daudi na watu wake ili kuwakamata.+
10 Sasa Absalomu akatuma wapelelezi+ katika nchi yote ya Israeli, akisema: “Mara mtakaposikia sauti ya baragumu, ninyi pia mseme, ‘Absalomu amekuwa mfalme+ katika Hebroni!’”+