36 Tazama! Huko pamoja nao kuna wana wao wawili, Ahimaazi+ wa Sadoki na Yonathani+ wa Abiathari; nanyi mwatumie hao kuniletea kila jambo ambalo huenda mkalisikia.”
16 Na sasa tuma ujumbe haraka na umwambie Daudi,+ ukisema, ‘Usiku wa leo usilale katika nchi tambarare za jangwa la nyikani, lakini wewe pia usikose kuvuka,+ ili mfalme na watu wote walio pamoja naye wasije wakamezwa.’”+
21 Na ikawa kwamba baada ya kuondoka kwao, ndipo wakatoka ndani ya kile kisima, wakaenda, wakamweleza Daudi na kumwambia Daudi: “Ondokeni, vukeni juu ya maji mbiombio; kwa maana hivi ndivyo Ahithofeli alivyotoa shauri+ juu yenu.”