10 Basi nikasimama juu yake na kwa hakika nikamuua,+ kwa maana nilijua kwamba hangeishi baada ya kuanguka. Kisha nikachukua taji+ lililokuwa juu ya kichwa chake na kikuku kilichokuwa kwenye mkono wake, ili nivilete kwa bwana wangu hapa.”
30 Naye akachukua taji la Malkamu kutoka juu ya kichwa chake,+ ambalo uzito wake ulikuwa talanta moja ya dhahabu, pamoja na mawe ya thamani; nalo likaja kuwa juu ya kichwa cha Daudi. Na nyara+ za jiji lile ambazo alileta zilikuwa nyingi sana.