3Naye Eliashibu+ kuhani mkuu na ndugu zake, makuhani, wakaondoka na kujenga Lango la Kondoo.+ Wao wenyewe walilitakasa+ na kuisimamisha milango yake; wakalitakasa mpaka kwenye Mnara wa Mea,+ mpaka Mnara wa Hananeli.+
6 Naye Yoyada mwana wa Pasea na Meshulamu mwana wa Besodeya wakarekebisha Lango la Jiji la Kale;+ wao walilijenga kwa mbao na kuisimamisha milango yake na komeo zake na mapingo+ yake.
13 Hanuni na wakaaji wa Zanoa+ wakarekebisha Lango la Bonde;+ wao wenyewe walilijenga na kuisimamisha milango+ yake, makomeo+ yake na mapingo+ yake, na pia urefu wa mikono elfu moja katika ukuta mpaka kwenye Lango la Marundo ya Majivu.+