10 Kisha Musa na Haruni wakaliita kutaniko pamoja mbele ya mwamba, naye akawaambia: “Sikieni, sasa, enyi waasi!+ Je, tuwatolee ninyi maji katika mwamba huu?”+
10 Lakini yeye akamwambia: “Wewe unasema kama anavyosema mmoja wa hao wanawake wasio na akili.+ Je, tukubali yaliyo mema tu kutoka kwa Mungu wa kweli, wala tusikubali pia yaliyo mabaya?”+ Katika hayo yote Ayubu hakutenda dhambi kwa midomo yake.+
2 Kwa maana sisi sote hujikwaa mara nyingi.+ Ikiwa yeyote hajikwai katika neno,+ huyo ni mtu mkamilifu,+ anayeweza kuuongoza kwa lijamu mwili wake wote pia.