Methali
16 Mipango ya moyo ni ya mtu wa udongo,+ lakini jibu la ulimi hutoka kwa Yehova.+
2 Njia zote za mwanadamu ni safi machoni pake mwenyewe,+ lakini Yehova anazipima roho.+
3 Mkabidhi Yehova mwenyewe kazi zako+ nayo mipango yako itafanywa imara.+
4 Yehova amefanya kila kitu kwa kusudi lake,+ naam, hata mwovu kwa ajili ya siku ya uovu.+
5 Kila mtu mwenye kiburi moyoni ni chukizo kwa Yehova.+ Mkono unaweza kuungana na mkono, hata hivyo mtu hatakosa adhabu.+
6 Kosa hufanyiwa upatanisho kwa fadhili zenye upendo na ukweli,+ na mtu huepuka uovu kwa kumwogopa Yehova.+
7 Yehova anapofurahia njia za mtu,+ huwafanya hata adui zake wawe na amani naye.+
8 Afadhali kuwa na kidogo pamoja na uadilifu+ kuliko kuwa na wingi pasipo haki.+
9 Huenda moyo wa mtu wa udongo ukaifikiria njia yake,+ lakini Yehova ndiye huzielekeza hatua zake.+
10 Uamuzi ulioongozwa na roho unapaswa kuwa katika midomo ya mfalme;+ kinywa chake hakipasi kukosa uaminifu katika hukumu.+
11 Kitu cha kupimia cha haki na mizani ni vya Yehova;+ mawe yote ya mizani ya mfuko ni kazi yake.+
12 Kufanya uovu ni chukizo kwa wafalme,+ kwa maana kiti cha ufalme hufanywa imara kwa uadilifu.+
13 Midomo ya uadilifu ni furaha ya mfalme mkuu;+ naye humpenda mtu anayesema mambo ya unyoofu.+
14 Ghadhabu ya mfalme ni kama wajumbe wa kifo,+ lakini mwenye hekima huigeuza.+
15 Katika nuru ya uso wa mfalme kuna uzima,+ nayo nia yake njema ni kama wingu la majira ya mvua ya masika.+
16 Kupata hekima ni bora kama nini kuliko dhahabu!+ Na kupata uelewaji kunapasa kuchaguliwa kuliko fedha.+
17 Njia kuu ya wanyoofu ni kuepuka ubaya.+ Anayeilinda njia yake anaitunza nafsi yake.+
18 Kiburi hutangulia kuanguka,+ na roho ya majivuno hutangulia kujikwaa.+
19 Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu+ pamoja na wapole kuliko kugawanya nyara pamoja na watu wanaojiinua.+
20 Anayetumia ufahamu katika jambo atapata mema,+ naye anayemtegemea Yehova+ ni mwenye furaha.
21 Mtu mwenye hekima moyoni itasemwa kwamba ana uelewaji,+ naye mwenye midomo mitamu huongeza ushawishi.+
22 Ufahamu ni kisima cha uzima+ kwa hao walio nao; nayo nidhamu ya wapumbavu ni upumbavu.+
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hukifanya kinywa chake kionyeshe ufahamu,+ na kwenye midomo yake huongeza ushawishi.+
24 Maneno yenye kupendeza ni sega la asali,+ ni matamu kwa nafsi na maponyo mifupani.+
25 Kuna njia ambayo imenyooka mbele ya mwanadamu,+ lakini njia za kifo ndizo mwisho wake baadaye.+
26 Nafsi ya mfanyakazi mwenye bidii imemfanyia kazi kwa bidii,+ kwa sababu kinywa chake kimemkaza sana.+
27 Mtu asiyefaa kitu anachimbua lililo baya,+ na katika midomo yake ni kana kwamba kuna moto unaounguza.+
28 Mtu mwenye hila huendelea kutokeza ugomvi nyakati zote,+ na mchongezi anawatenganisha wale wanaofahamiana.+
29 Mtu wa jeuri atamshawishi mwenzake,+ naye hakika humfanya aende katika njia isiyo njema.+ 30 Anakonyeza-konyeza macho yake ili kupanga hila.+ Akikaza midomo yake, hakika yeye hukamilisha madhara.
31 Kichwa chenye mvi ni taji la uzuri+ kinapopatikana katika njia ya uadilifu.+
32 Asiye mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwanamume mwenye nguvu,+ naye anayezuia roho yake ni bora kuliko mtu anayeteka jiji.+
33 Watu hutupa kura ndani ya mkunjo wa nguo,+ lakini kila uamuzi unaofanywa kupitia kura hiyo hutoka kwa Yehova. +