Mambo ya Walawi 19:36 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 36 Mtakuwa na mizani sahihi, vipimo sahihi,+ kipimo sahihi cha efa na kipimo sahihi cha hini. Mimi ni Yehova Mungu wenu, ambaye nimewatoa ninyi katika nchi ya Misri. Methali 11:1 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 11 Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa Yehova,+ lakini jiwe kamili la mizani ni furaha kwake. Ezekieli 45:10 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 10 ‘Mnapaswa kuwa na mizani sahihi na efa sahihi na kipimo sahihi cha bathi.+
36 Mtakuwa na mizani sahihi, vipimo sahihi,+ kipimo sahihi cha efa na kipimo sahihi cha hini. Mimi ni Yehova Mungu wenu, ambaye nimewatoa ninyi katika nchi ya Misri.