Methali
11 Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa Yehova,+ lakini jiwe kamili la mizani ni furaha kwake.
2 Je, kimbelembele kimekuja? Basi aibu itakuja;+ lakini wenye kiasi wana hekima.+
3 Utimilifu wa wanyoofu ndio huwaongoza,+ lakini upotovu wa wale wanaotenda kwa hila utawaharibu.+
4 Vitu vyenye thamani havitakuwa na faida yoyote siku ya ghadhabu,+ lakini uadilifu utakomboa kutoka katika kifo.+
5 Uadilifu wa mtu asiye na lawama ndio utakaoinyoosha njia yake,+ lakini mwovu ataanguka katika uovu wake mwenyewe.+ 6 Uadilifu wa wanyoofu ndio utakaowakomboa,+ lakini wale wanaotenda kwa hila wao wenyewe watakamatwa kwa tamaa yao.+
7 Mwovu anapokufa, tumaini lake hupotea;+ na hata tarajio linalotegemea nguvu limepotea.+
8 Mwadilifu ndiye huokolewa kutoka katika taabu,+ na mwovu huingia badala yake.+
9 Mwasi-imani humletea mwenzake uharibifu kwa kinywa chake,+ lakini waadilifu huokolewa kwa ujuzi.+
10 Mji huchangamka kwa sababu ya wema wa waadilifu,+ lakini watu hulia kwa shangwe waovu wanapoangamia.+
11 Mji huinuliwa kwa sababu ya baraka ya wanyoofu,+ lakini hubomolewa kwa sababu ya kinywa cha waovu.+
12 Mtu ambaye amepungukiwa moyoni amemdharau mwenzake,+ lakini mtu mwenye utambuzi mwingi hukaa kimya.+
13 Mtu anayetembea huku na huku akiwa mchongezi+ anafunua mazungumzo ya siri,+ lakini mtu mwaminifu katika roho anafunika jambo.+
14 Wakati ambapo hakuna mwongozo stadi, watu huanguka;+ lakini kwa wingi wa washauri kuna wokovu.+
15 Mtu ambaye amemwekea dhamana mgeni+ hakika atapatwa na mabaya, lakini anayechukia kufanya mapatano kwa kupeana mkono hukaa bila wasiwasi.
16 Mwanamke mwenye kuvutia ndiye anayepata utukufu;+ lakini watu wenye kuonea, kwa upande wao, hupata utajiri.
17 Mwanamume mwenye fadhili zenye upendo anaitendea kwa kuipa thawabu nafsi yake mwenyewe,+ lakini mtu mkatili anajiletea taabu.+
18 Mtu mwovu anapata mshahara wa uwongo,+ lakini anayepanda uadilifu, hupata mapato ya kweli.+
19 Anayesimama imara kwa ajili ya uadilifu anaelekea kupata uzima,+ lakini anayefuatilia yaliyo mabaya anaelekea kwenye kifo chake mwenyewe.+
20 Waliopotoka moyoni ni chukizo kwa Yehova,+ lakini wasio na lawama katika njia yao ni furaha kwake.+
21 Mkono ujaposhikana na mkono, mtu mbaya hatakosa kupewa adhabu;+ lakini uzao wa waadilifu hakika utaponyoka.+
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe, ndivyo alivyo mwanamke mwenye umbo la kupendeza lakini anayegeuka na kuacha kuwa na akili.+
23 Tamaa ya waadilifu hakika ni njema;+ tumaini la waovu ni ghadhabu.+
24 Kuna mtu anayetawanya na bado anaongezewa;+ pia kuna mtu anayewanyima wengine yaliyo sawa, lakini hilo huleta uhitaji tu.+
25 Nafsi yenye ukarimu hiyo yenyewe itanoneshwa,+ naye anayenywesha wengine kwa ukarimu yeye mwenyewe pia atanyweshwa kwa ukarimu.+
26 Anayewanyima watu nafaka—watu watamlaani, lakini kuna baraka kwa ajili ya kichwa cha mtu anayekubali inunuliwe.+
27 Anayetafuta mema ataendelea kutafuta nia njema;+ lakini anayetafuta ubaya, huo utamjia.+
28 Anayetegemea utajiri wake—yeye mwenyewe ataanguka;+ lakini waadilifu watasitawi kama majani.+
29 Yeyote anayeiletea nyumba yake taabu,+ ataumiliki upepo;+ na mtu mpumbavu atakuwa mtumishi wa mtu mwenye hekima moyoni.
30 Matunda ya mwadilifu ni mti wa uzima,+ naye anayevuta nafsi za watu ni mwenye hekima.+
31 Tazama! Mtu mwadilifu—katika dunia atapewa thawabu.+ Basi mwovu na mtenda-dhambi watapewa thawabu hata zaidi!+