Methali
15 Jibu, linapokuwa la upole, hugeuza ghadhabu,+ lakini neno linaloumiza hufanya hasira ipande.+
2 Ulimi wa watu wenye hekima hutenda mema kwa ujuzi,+ lakini kinywa cha wajinga hububujika upumbavu.+
3 Macho ya Yehova yako kila mahali,+ yakiwaangalia wabaya na wema.+
4 Utulivu wa ulimi ni mti wa uzima,+ lakini upotovu wake humaanisha kuvunjika katika roho.+
5 Yeyote aliye mpumbavu hudharau nidhamu ya baba yake,+ lakini mtu yeyote anayejali karipio ni mwerevu.+
6 Katika nyumba ya mwadilifu mna akiba nyingi,+ lakini katika mazao ya mwovu mna taabu.+
7 Midomo ya watu wenye hekima hutawanya ujuzi sikuzote,+ lakini moyo wa wajinga hauko hivyo.+
8 Dhabihu ya waovu ni chukizo kwa Yehova,+ lakini sala ya wanyoofu ni furaha kwake.+
9 Njia ya mwovu ni chukizo kwa Yehova,+ lakini humpenda mtu anayefuatilia uadilifu.+
10 Nidhamu ni mbaya kwa mtu anayeiacha njia;+ mtu yeyote anayechukia karipio atakufa.+
11 Kaburi* na mahali pa maangamizi+ viko mbele za Yehova.+ Basi, mioyo ya wana wa binadamu+ ni zaidi!
12 Mwenye dhihaka hampendi mtu anayemkaripia.+ Yeye hataenda kwa watu wenye hekima.+
13 Moyo wenye shangwe huchangamsha sura,+ lakini kwa sababu ya maumivu ya moyo roho hupata pigo.+
14 Moyo wa uelewaji hutafuta ujuzi,+ lakini kinywa cha watu wajinga hutafuta upumbavu.+
15 Siku zote za mwenye kuteseka ni mbaya,+ lakini mtu aliye mchangamfu moyoni huwa na karamu sikuzote.+
16 Afadhali kuwa na vitu vichache pamoja na kumwogopa Yehova+ kuliko kuwa na vitu vingi pamoja na mvurugo.+
17 Afadhali chakula cha mboga za majani mahali penye upendo+ kuliko ng’ombe-dume aliyenoneshwa pamoja na chuki.+
18 Mtu mwenye ghadhabu huchochea ugomvi,+ lakini yule ambaye hakasiriki upesi hutuliza mabishano.+
19 Njia ya mvivu ni kama boma la miiba,+ lakini mapito ya wanyoofu ni njia iliyofanywa kuwa laini.+
20 Mwana mwenye hekima ndiye humfanya baba yake ashangilie,+ lakini mtu mjinga anamdharau mama yake.+
21 Mtu ambaye amepungukiwa moyoni huonea shangwe upumbavu,+ lakini mtu mwenye utambuzi huenda mbele moja kwa moja.+
22 Mipango huvunjika mahali ambapo hapana mazungumzo ya siri,+ lakini katika wingi wa washauri mambo hutimizwa.+
23 Mtu hushangilia jibu la kinywa chake,+ nalo neno linalosemwa wakati unaofaa ni jema kama nini!+
24 Kwa yule anayetenda kwa ufahamu njia ya uzima inaelekea juu,+ ili kuliepuka Kaburi* lililo chini.+
25 Yehova ataibomoa nyumba ya watu waliojiinua,+ lakini atauweka imara mpaka wa mjane.+
26 Hila za mtu mbaya ni chukizo kwa Yehova,+ lakini maneno yenye kupendeza ni safi.+
27 Mtu anayepata faida isiyo ya haki anailetea nyumba yake mwenyewe taabu,+ lakini anayechukia zawadi ndiye atakayeendelea kuishi.+
28 Moyo wa mwadilifu hutafakari ili kujibu,+ lakini kinywa cha waovu hububujika mambo mabaya.+
29 Yehova yuko mbali sana na waovu,+ lakini huisikia sala ya waadilifu.+
30 Kung’aa kwa macho+ hufanya moyo ushangilie;+ habari+ ambayo ni njema huifanya mifupa inone.+
31 Sikio linalosikiliza karipio+ la uzima hukaa kati ya watu wenye hekima.+
32 Yeyote anayeepuka nidhamu+ anaikataa nafsi yake mwenyewe, lakini anayesikiliza karipio anajipatia utambuzi wa moyo.+
33 Kumwogopa Yehova ni nidhamu ya hekima,+ na kabla ya utukufu hutangulia unyenyekevu.+