Methali
17 Afadhali kipande kikavu cha mkate pamoja na utulivu+ kuliko nyumba iliyojaa dhabihu za kugombana.+
2 Mtumishi anayeonyesha ufahamu atamtawala mwana anayetenda kwa aibu,+ na kati ya ndugu atapata sehemu ya urithi.+
3 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,+ lakini Yehova ndiye mchunguzaji wa mioyo.+
4 Mtenda-maovu anasikiliza kwa makini mdomo wenye madhara.+ Mwongo anatega sikio asikilize ulimi unaotokeza shida.+
5 Anayemdhihaki maskini anamletea shutuma Mtengenezaji+ wake. Anayeshangilia msiba wa mwingine hatakosa adhabu.+
6 Taji la wazee ni wajukuu,+ na uzuri wa wana ni baba zao.+
7 Mdomo wa unyoofu haumstahili mtu asiye na akili.+ Sembuse mdomo wa uwongo kwa mtu mwenye kuheshimika!+
8 Zawadi ni jiwe la thamani linaloleta kibali machoni pa yule aliye nayo.+ Kila mahali anapogeukia anafanikiwa.+
9 Anayefunika makosa anatafuta upendo,+ naye anayeendelea kuongea juu ya jambo anawatenganisha watu wanaofahamiana.+
10 Kemeo huingia ndani zaidi katika mtu mwenye uelewaji+ kuliko kumpiga mjinga mara mia moja.+
11 Mtu mbaya huendelea kutafuta uasi tu,+ na mjumbe anayetumwa kwake ni mkatili.+
12 Afadhali mtu akutane na dubu aliyepoteza watoto wake+ kuliko kukutana na mjinga katika upumbavu wake.+
13 Mtu anayelipa ubaya kwa wema,+ ubaya hautaondoka nyumbani mwake.+
14 Mwanzo wa ugomvi ni kama mtu anayefungulia maji;+ kwa hiyo kabla mabishano hayajalipuka, jiondokee.+
15 Yeyote anayemtangaza mwovu kuwa mwadilifu+ na yeyote anayemtangaza mwadilifu kuwa mwovu+—wote wawili ni chukizo kwa Yehova.+
16 Kwa nini mjinga ana uwezo mkononi mwake wa kujipatia hekima,+ hali yeye hana utambuzi wa moyo?+
17 Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote,+ naye ni ndugu aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.+
18 Mtu aliyepungukiwa moyoni hupeana mikono,+ akitoa dhamana kamili mbele ya mwenzake.+
19 Mtu anayependa makosa anapenda mashindano.+ Mtu anayeinua mahali pake pa kuingilia anatafuta kuanguka.+
20 Mtu mwenye moyo mpotovu hatapata mema,+ naye anayebadilika-badilika kwa ulimi ataanguka katika msiba.+
21 Yeyote anayezaa mtoto mjinga—ni huzuni kwake;+ na baba ya mtoto asiye na akili hana shangwe.+
22 Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri,+ lakini roho iliyopondeka huikausha mifupa.+
23 Mwovu atachukua hata rushwa kifuani+ ili kupotosha mapito ya hukumu.+
24 Hekima iko mbele ya uso wa mtu mwenye uelewaji,+ lakini macho ya mjinga yako kwenye mwisho wa dunia.+
25 Mwana mjinga ni huzuni kwa baba yake+ na ni uchungu kwa mama aliyemzaa.+
26 Zaidi ya hayo, si vema kumtoza mwadilifu.+ Kuwapiga watu wenye kuheshimika ni kinyume cha jambo lililonyooka.+
27 Yeyote anayezuia maneno yake ana ujuzi,+ na mtu mwenye utambuzi ana roho ya utulivu.+
28 Hata mtu mpumbavu, anapokaa kimya, ataonwa kuwa mwenye hekima;+ yeyote anayefunga midomo yake, ataonwa kuwa mwenye uelewaji.