Methali
18 Mtu anayejitenga na wengine atatafuta mapendezi yake mwenyewe;+ atashindana na hekima yote inayotumika.+
2 Yeyote aliye mjinga hapendezwi na utambuzi hata kidogo,+ isipokuwa tu moyo wake ujifunue wenyewe.+
3 Mwovu anapoingia, dharau huingia pia;+ na ukosefu wa heshima+ huwa pamoja na shutuma.
4 Maneno ya kinywa cha mwanadamu ni kilindi cha maji.+ Kisima cha hekima ni kijito cha maji yanayobubujika.+
5 Si vema kumwonyesha mwovu upendeleo,+ wala kumpotosha mwadilifu katika hukumu.+
6 Midomo ya mtu aliye mjinga huingia katika mabishano,+ na kinywa chake huitisha mapigo.+
7 Kinywa cha mjinga ni uharibifu wake,+ na midomo yake ni mtego wa nafsi yake.+
8 Maneno ya mchongezi ni kama vitu vya kumezwa kwa pupa,+ vinavyoingia katika sehemu za ndani kabisa za tumbo.+
9 Pia, mtu anayejionyesha kuwa mvivu katika kazi yake+—yeye ni ndugu ya mtu anayeleta uharibifu.+
10 Jina la Yehova ni mnara wenye nguvu.+ Mwadilifu hukimbilia humo na kupewa ulinzi.+
11 Vitu vyenye thamani vya tajiri ni mji wake wenye nguvu,+ navyo ni kama ukuta wa ulinzi katika mawazo yake.+
12 Kabla ya kuanguka moyo wa mwanadamu huwa na kiburi,+ na kabla ya utukufu kuna unyenyekevu.+
13 Yeyote anapojibu jambo kabla ya kulisikia,+ huo ni upumbavu na aibu kwake.+
14 Roho ya mwanadamu inaweza kuvumilia ugonjwa wake;+ lakini ni nani anayeweza kuvumilia roho iliyopondeka?+
15 Moyo wa mtu mwenye uelewaji hujipatia ujuzi,+ nalo sikio la wenye hekima hutafuta kupata ujuzi.+
16 Zawadi ya mwanadamu itamfungulia nafasi kubwa,+ nayo itamwongoza hata mbele ya watu wakuu.+
17 Mtu wa kwanza katika kesi yake ni mwadilifu;+ mwenzake huingia naye hakika humchunguza kwa undani.+
18 Kura hutuliza hata magomvi,+ nayo huwatenganisha hata watu wenye nguvu.+
19 Ndugu aliyekosewa ni mgumu kuliko mji wenye nguvu;+ na kuna magomvi yaliyo kama pingo la mnara wa makao.+
20 Kutokana na matunda ya kinywa cha mtu, tumbo lake litashiba;+ atashiba hata mazao ya midomo yake.+
21 Kifo na uzima viko katika nguvu za ulimi,+ naye anayeupenda atakula matunda yake.+
22 Je, mtu amepata mke mwema?+ Amepata kitu chema,+ na mtu hupata nia njema kutoka kwa Yehova.+
23 Maskini husema kwa kusihi,+ lakini tajiri hujibu kwa ukali.+
24 Kuna rafiki wanaoelekea kuvunjana vipande-vipande,+ lakini yuko rafiki anayeshikamana na mtu kwa ukaribu zaidi kuliko ndugu.+