7 Lakini Yehova akamwambia Samweli: “Usiangalie sura yake wala urefu+ wa umbo lake, kwa maana nimemkataa. Kwa kuwa Mungu haoni kama mwanadamu anavyoona,+ kwa maana mwanadamu huona kile kinachoonekana kwa macho,+ lakini Yehova huona jinsi moyo+ ulivyo.”
12 Ikiwa utasema: “Tazama! Hatukujua hili,”+ je, yule anayeipima mioyo hatatambua hilo,+ na yule anayeichunguza nafsi yako mwenyewe hatajua+ hilo naye hakika hatamlipa mtu wa udongo kulingana na utendaji wake?+
15 Kwa hiyo akawaambia: “Ninyi ni wale mnaojitangaza kuwa waadilifu mbele ya macho ya wanadamu,+ lakini Mungu anaijua mioyo+ yenu; kwa sababu kilichoinuka sana kati ya wanadamu ni chukizo machoni pa Mungu.+