13 Lakini akamwambia: “Bwana wangu anajua kwamba hawa watoto ni dhaifu na kondoo na ng’ombe wanaonyonyesha wako chini ya usimamizi wangu.+ Nao wakiwaendesha haraka mno kwa siku moja, basi kundi zima litakufa bila shaka.+
12 “Siku sita utafanya kazi yako;+ lakini siku ya saba utaacha, ili ng’ombe-dume wako na punda wako wapate kupumzika na mwana wa kijakazi wako na mkaaji mgeni wapate kujiburudisha.+
11 Na mimi, kwa upande wangu, je, sipaswi kusikitikia Ninawi lile jiji kubwa,+ ambalo lina wanadamu zaidi ya 120,000 wasiojua hata kidogo tofauti kati ya mkono wao wa kuume na wa kushoto, na tena wanyama wengi wa kufugwa?”+