17 Pia, atakwenda mbele zake kwa roho na nguvu za Eliya,+ ili kurudisha mioyo+ ya akina baba kwa watoto na wale wasiotii kwenye hekima inayotumika ya waadilifu, ili kuweka tayari kwa ajili ya Yehova+ watu waliotayarishwa.”+
8 Na bwana wake akamsifu yule msimamizi, kwa sababu alikuwa ametenda kwa hekima inayotumika,+ ingawa si mwadilifu; kwa maana wana wa mfumo huu wa mambo wana hekima zaidi kwa njia inayotumika kuelekea kizazi chao wenyewe kuliko vile walivyo wana wa nuru.+