Methali
3 Mwanangu, usiisahau sheria yangu,+ na moyo wako upate kushika amri zangu,+ 2 kwa sababu utaongezewa+ urefu wa siku na miaka ya uzima+ na amani. 3 Fadhili zenye upendo na ukweli zisikuache.+ Zifunge shingoni pako.+ Ziandike kwenye kibao cha moyo wako,+ 4 na hivyo upate kibali na ufahamu mzuri machoni pa Mungu na machoni pa mtu wa udongo.+ 5 Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote+ wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe.+ 6 Mtambue yeye katika njia zako zote,+ naye atanyoosha mapito yako.+
7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe.+ Mwogope Yehova na ujiepushe na ubaya.+ 8 Na hilo liwe maponyo+ kwenye kitovu chako na burudisho kwa mifupa yako.+
9 Mheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye thamani+ na kwa matunda ya kwanza ya mazao yako yote.+ 10 Ndipo maghala yako yatakapojazwa kwa wingi;+ nayo mitungi yako ya shinikizo itafurika divai mpya.+
11 Ewe mwanangu, usikatae nidhamu ya Yehova;+ wala usichukie karipio lake,+ 12 kwa sababu yeye ambaye Yehova anampenda,+ humkaripia, kama vile baba anavyomkaripia mwana anayemfurahia.+
13 Mwenye furaha ni mtu ambaye amepata hekima,+ na mtu anayepata utambuzi,+ 14 kwa maana kuwa nayo kama mapato ni bora kuliko kuwa na mapato ya fedha na kuwa nayo kama mazao ni bora kuliko dhahabu+ yenyewe. 15 Ina thamani kuliko marijani,+ na mapendezi yako mengine yote hayawezi kulinganishwa nayo. 16 Urefu wa siku uko katika mkono wake wa kuume;+ na katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na utukufu.+ 17 Njia zake ni njia za uzuri, na barabara zake zote ni amani.+ 18 Ni mti wa uzima+ kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana+ wataitwa wenye furaha.+
19 Kwa hekima Yehova mwenyewe aliuweka msingi wa dunia.+ Aliziweka mbingu imara kwa utambuzi.+ 20 Kwa ujuzi wake vilindi vya maji vilitenganishwa,+ nazo anga zenye mawingu hutoa matone ya mvua nyepesi.+ 21 Mwanangu, zisiondoke machoni pako.+ Linda hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri,+ 22 nazo zitakuwa uzima kwa nafsi yako+ na kitu chenye kuvutia shingoni pako.+ 23 Ndipo utakapotembea kwa usalama+ njiani mwako, na hata mguu wako hautagonga chochote.+ 24 Unapolala hutahofu;+ nawe hakika utalala, nao usingizi wako utakuwa mtamu.+ 25 Hutaogopa kitu chochote chenye kuogopesha ghafula,+ wala dhoruba inayowajia waovu, kwa sababu inakuja.+ 26 Kwa maana Yehova mwenyewe atakuwa uhakika wako,+ naye hakika ataepusha mguu wako usinaswe.+
27 Usiwanyime watu mema wanayostahili,+ mkono wako ukiwa na uwezo wa kuyafanya.+ 28 Usimwambie mwenzako: “Nenda, kisha urudi na kesho nitakupa,” na kumbe una kitu anachohitaji.+ 29 Usimtungie mwenzako jambo lolote baya,+ wakati anapokaa nawe na kujiona salama.+ 30 Usigombane na mtu bila sababu,+ ikiwa hajakufanyia ubaya wowote.+
31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri,+ wala kuchagua yoyote kati ya njia zake.+ 32 Kwa maana mtu mwenye hila+ ni chukizo kwa Yehova,+ lakini urafiki Wake uko pamoja na watu wanyoofu.+ 33 Laana ya Yehova iko juu ya nyumba ya mwovu,+ lakini huyabariki makao ya waadilifu.+ 34 Atawadhihaki+ wale wenye dhihaka;+ lakini atawapa wapole kibali.+ 35 Wenye hekima watapata heshima,+ lakini wajinga wanainua aibu.+