Methali
2 Mwanangu, ikiwa utapokea maneno yangu+ na kujiwekea amri zangu kama hazina,+ 2 ili kwa sikio lako usikilize hekima kwa makini,+ ili uelekeze moyo wako kwenye utambuzi,+ 3 ikiwa utaita uelewaji+ na kupaaza sauti yako uite utambuzi,+ 4 ikiwa utaendelea kuutafuta kama fedha,+ na kuendelea kuutafuta kama hazina zilizofichika,+ 5 ndipo utakapoelewa kumwogopa+ Yehova, nawe utapata kumjua Mungu.+ 6 Kwa maana Yehova mwenyewe anatoa hekima;+ kinywani mwake hutoka ujuzi na utambuzi.+ 7 Naye atawawekea wanyoofu hazina ya hekima inayotumika;+ yeye ni ngao kwa wale wanaotembea kwa utimilifu,+ 8 kwa kushika mapito ya hukumu,+ naye atailinda njia ya washikamanifu wake.+ 9 Ndipo utakapoelewa uadilifu na hukumu na unyoofu, njia yote ya yaliyo mema.+
10 Hekima inapoingia moyoni mwako+ na ujuzi kupendeza nafsi yako,+ 11 uwezo wa kufikiri utakutunza,+ utambuzi utakulinda,+ 12 ili kukukomboa kutoka katika njia mbaya,+ na kutoka kwa mtu anayesema mambo mapotovu,+ 13 kutoka kwa wale wanaoacha mapito ya unyoofu ili watembee katika njia za giza,+ 14 kutoka kwa wale wanaofurahia kufanya mabaya,+ wanaoshangilia mambo mapotovu ya ubaya;+ 15 wale ambao mapito yao yamepotoka na ambao kwa ujumla ni wenye hila maishani mwao;+ 16 ili huo ukukomboe kutoka kwa mwanamke, naam, kutoka kwa mwanamke mgeni+ ambaye amefanya maneno yake kuwa laini,+ 17 anayemwacha rafiki wa ujana wake+ na ambaye amelisahau agano la Mungu wake.+ 18 Kwa maana nyumba yake huzama ndani ya kifo na mapito yake huzama ndani kwa wale wasiojiweza katika kifo.+ 19 Hakuna yeyote kati ya wale wanaolala naye atakayerudi, wala hawatayafikia tena mapito ya walio hai.+
20 Kusudi ni kwamba upate kutembea katika njia ya watu wema+ na kwamba upate kushika mapito ya waadilifu.+ 21 Kwa maana wanyoofu ndio watakaokaa duniani,+ na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake.+ 22 Nao waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani;+ nao wenye hila, watang’olewa kutoka ndani yake.+