Methali
Methali
1 Methali+ za Sulemani+ mwana wa Daudi,+ mfalme wa Israeli,+ 2 ili mtu ajue hekima+ na nidhamu,+ na kutambua maneno ya uelewaji,+ 3 apokee nidhamu+ ambayo humpa mtu ufahamu,+ uadilifu+ na haki+ na unyoofu,+ 4 kuwapa werevu wale wasio na uzoefu,+ kumpa kijana ujuzi+ na uwezo wa kufikiri.+
5 Mtu mwenye hekima atasikiliza na kupata mafundisho zaidi,+ naye mtu mwenye uelewaji ndiye anayepata mwongozo stadi,+ 6 ili kuelewa methali na mafumbo,+ maneno ya watu wenye hekima+ na vitendawili vyao.+
7 Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa ujuzi.+ Wapumbavu wamedharau hekima na nidhamu.+
8 Mwanangu, sikiliza nidhamu ya baba yako,+ wala usiiache sheria ya mama yako.+ 9 Kwa maana hizo ni shada lenye kuvutia kichwani pako+ na mkufu bora shingoni pako.+
10 Mwanangu, watenda-dhambi wakijaribu kukushawishi, usikubali.+ 11 Wakizidi kusema: “Haya, njoo pamoja nasi. Na tuvizie ili kumwaga damu.+ Na tujifiche ili kuwashambulia, bila sababu, watu wasio na hatia.+ 12 Na tuwameze wakiwa hai+ kama Kaburi,*+ naam, wakiwa wazima, kama wale wanaoshuka shimoni.+ 13 Na tupate namna zote za vitu vyenye thamani.+ Na tujaze nyara katika nyumba zetu.+ 14 Unapaswa kupiga kura yako katikati yetu. Nasi sote tuwe na mfuko mmoja tu”+— 15 mwanangu, usiende njiani pamoja nao.+ Zuia mguu wako usiende katika barabara yao.+ 16 Maana miguu yao hukimbilia ubaya mtupu,+ nao huharakisha kwenda kumwaga damu.+ 17 Kwa maana wavu hutandikwa pasipo kusudi mbele ya macho ya kiumbe chochote chenye mabawa.+ 18 Basi wao wenyewe huwavizia ili kumwaga damu yao;+ hujificha ili wazishambulie nafsi zao.+ 19 Hayo ndiyo mapito ya kila mtu anayepata faida isiyo ya haki.+ Huiondoa nafsi yao walio nayo.+
20 Hekima ya kweli+ huendelea kulia kwa sauti kubwa barabarani.+ Hutoa sauti yake katika viwanja vya watu wote.+ 21 Inaita penye mwisho wa upande wa juu wa barabara yenye kelele.+ Husema maneno yake katika mahali pa kuingilia malango ya jiji:+
22 “Ninyi msio na uzoefu mtaendelea mpaka wakati gani kupenda kutokuwa na ujuzi?+ Nanyi wenye dhihaka mtaendelea mpaka wakati gani kujitakia dhihaka tupu?+ Nanyi wajinga mtaendelea mpaka wakati gani kuchukia ujuzi?+ 23 Geukeni mpate karipio langu.+ Ndipo mimi nitafanya roho yangu ibubujike juu yenu;+ nitawajulisha maneno yangu.+ 24 Kwa sababu nimewaita lakini mnaendelea kukataa.+ Nimenyoosha mkono wangu lakini hakuna yeyote anayetazama.+ 25 Nanyi mnazidi kupuuza mashauri yangu yote,+ wala hamkukubali karipio langu.+ 26 Mimi pia, kwa upande wangu, nitacheka taabu yenu wenyewe,+ na jambo mnalohofu litakapokuja nitafanya mzaha,+ 27 jambo mnalohofu litakapokuja kama dhoruba, na taabu yenu wenyewe itakapofika kama upepo wa dhoruba,+ na shida na nyakati ngumu zitakapowapata.+ 28 Wakati huo wataendelea kuniita, lakini sitaitika;+ wataendelea kunitafuta, lakini hawatanipata,+ 29 kwa sababu walichukia ujuzi,+ nao hawakuchagua kumwogopa Yehova.+ 30 Hawakukubali shauri langu;+ walipuuza makaripio yangu yote.+ 31 Basi watakula matunda ya njia yao,+ nao watashiba mashauri yao wenyewe.+ 32 Kwa maana uasi+ wa wasio na uzoefu utawaua wao,+ na kutojali kwa wajinga kutawaangamiza wao.+ 33 Kwa habari yake mtu anayenisikiliza, yeye atakaa salama+ wala hatasumbuliwa na hofu ya msiba.”+