Methali
8 Je, hekima haendelei kupaaza sauti,+ na utambuzi haendelei kutoa sauti yake?+ 2 Husimama juu ya vilele,+ kando ya njia, kwenye makutano ya barabara. 3 Kando ya malango, kinywani pa mji,+ kwenye kiingilio cha malango huendelea kulia kwa sauti kubwa:+
4 “Ninawaita ninyi, enyi watu, nayo sauti yangu inawaita wana wa binadamu.+ 5 Enyi msio na uzoefu, eleweni werevu;+ nanyi wajinga, eleweni utambuzi wa moyo.+ 6 Sikilizeni, kwa maana ninasema juu ya mambo ya kwanza kabisa,+ nami ninaifungua midomo yangu kuhusu unyoofu.+ 7 Kwa maana kaakaa langu husema ukweli wenyewe+ kwa sauti ya chini; na uovu ni chukizo kwa midomo yangu.+ 8 Maneno yote ya kinywa changu ni ya uadilifu.+ Kati ya hayo hamna jambo lililopotoka wala lililo kombo.+ 9 Yote hayo yamenyooka kwa mtu mwenye utambuzi, na ni ya unyoofu kwa wale wanaopata ujuzi.+ 10 Chukueni nidhamu yangu wala si fedha, na ujuzi badala ya dhahabu bora.+ 11 Kwa maana hekima ni bora kuliko marijani,+ na vitu vingine vyote vyenye kupendeza haviwezi kulinganishwa nayo.+
12 “Mimi, hekima, nimefanya makao pamoja na werevu+ nami napata hata ujuzi wa uwezo wa kufikiri.+ 13 Kumwogopa Yehova humaanisha kuchukia yaliyo mabaya.+ Nimechukia kujiinua na kiburi+ na njia mbaya na kinywa kipotovu.+ 14 Nina mashauri+ na hekima inayotumika.+ Mimi—uelewaji;+ nina uwezo.+ 15 Kwa msaada wangu wafalme wenyewe huendelea kutawala, na maofisa wakuu wenyewe huendelea kuagiza juu ya uadilifu.+ 16 Kwa msaada wangu wakuu wenyewe huendelea kutawala wakiwa wakuu,+ nao watu wote wenye vyeo wanahukumu katika uadilifu.+ 17 Wanaonipenda mimi ninawapenda,+ nao wanaonitafuta mimi ndio wanaonipata.+ 18 Nina utajiri na utukufu,+ vitu vya urithi vyenye thamani na uadilifu.+ 19 Matunda yangu ni bora kuliko dhahabu, hata kuliko dhahabu safi, nayo mazao yangu ni bora kuliko fedha bora.+ 20 Mimi hutembea katika njia ya uadilifu,+ katikati ya barabara za hukumu,+ 21 ili kuwafanya wanaonipenda wawe na vitu halisi;+ nami huendelea kujaza maghala yao.+
22 “Yehova mwenyewe alinitokeza nikiwa mwanzo wa njia yake,+ nikiwa wa mapema zaidi kati ya kazi zake za zamani za kale.+ 23 Niliwekwa tangu wakati usio na kipimo,+ tangu mwanzoni, tangu nyakati za mapema kabla ya dunia.+ 24 Wakati ambapo hakukuwa na vilindi vya maji nilitokezwa kana kwamba kwa uchungu wa kuzaa,+ wakati ambapo hakukuwa na chemchemi zilizojaa sana maji. 25 Kabla milima yenyewe haijawekwa,+ kabla ya vilima, nilitokezwa kana kwamba kwa uchungu wa kuzaa, 26 kabla hajaifanya dunia+ na nchi tambarare na sehemu ya kwanza ya mavumbi ya nchi yenye kuzaa.+ 27 Alipozitayarisha mbingu nilikuwako;+ alipoagiza mviringo juu ya uso wa kilindi cha maji,+ 28 alipoweka imara mawingu makubwa yaliyo juu,+ alipofanya chemchemi za kilindi cha maji ziwe na nguvu,+ 29 alipoiwekea bahari sheria yake kwamba maji yasipite agizo lake,+ alipoiweka misingi ya dunia,+ 30 ndipo nilipokuwa kando yake nikiwa stadi wa kazi,+ nami nikawa yule ambaye yeye alimpenda sana+ kwa njia ya pekee siku baada ya siku, nami nikawa nikifurahi mbele zake wakati wote,+ 31 nikifurahi kwa sababu ya dunia yake yenye kutoa mazao,+ na vitu nilivyopenda sana vilihusiana na wana wa binadamu.+
32 “Na sasa, enyi wana, nisikilizeni; naam, wenye furaha ni wale wanaoshika njia zangu.+ 33 Sikiliza nidhamu upate kuwa na hekima,+ wala usipuuze hata kidogo.+ 34 Mwenye furaha ni yule anayenisikiliza kwa kukaa macho milangoni pangu siku baada ya siku, kwa kulinda kwenye vizingiti vya mahali pangu pa kuingilia.+ 35 Kwa maana anayenipata hakika atapata uzima,+ naye hupata nia njema kutoka kwa Yehova.+ 36 Lakini anayekosa kunipata anaifanyia nafsi yake jeuri;+ wale wote wanaonichukia vikali ndio wanaopenda kifo.”+