Methali
7 Mwanangu, shika maneno yangu,+ na uzitunze amri zangu kama hazina.+ 2 Shika amri zangu uendelee kuishi,+ na sheria yangu kama mboni+ ya macho yako. 3 Zifunge juu ya vidole vyako,+ na kuziandika juu ya kibao cha moyo wako.+ 4 Iambie hekima:+ “Wewe ni dada yangu”; na uite uelewaji “Mwanamke wa ukoo wangu,” 5 ili kukulinda na mwanamke mgeni,+ na mwanamke wa kigeni ambaye amefanya maneno yake mwenyewe kuwa laini.+ 6 Kwa maana penye dirisha la nyumba yangu, kupitia pazia+ langu nilitazama chini, 7 ili kuwachungulia wasio na uzoefu.+ Nilipendezwa kutambua kati ya wana, kijana ambaye amepungukiwa moyoni,+ 8 akipita barabarani, karibu na pembeni kwa mwanamke huyo, naye kijana huyo akashika njia inayoenda nyumbani kwa mwanamke huyo,+ 9 wakati wa gizagiza, jioni ya siku hiyo,+ usiku ukikaribia kuingia na kukiwa na giza. 10 Na, tazama! mwanamke akaja kumpokea, mwenye vazi la kahaba+ na ujanja wa moyo. 11 Yeye ni mwanamke mwenye msukosuko na mkaidi.+ Miguu yake haikai nyumbani mwake.+ 12 Mara yuko nje, mara yuko katika viwanja vya watu wote,+ naye huvizia karibu na kila pembe.+ 13 Naye mwanamke huyo akamkamata yule kijana na kumbusu.+ Huyo mwanamke ana uso usio na haya, naye akaanza kumwambia yule kijana:
14 “Nilipaswa kutoa dhabihu za ushirika.+ Leo nimetimiza nadhiri zangu.+ 15 Ndiyo sababu nimekuja kukupokea, niutafute uso wako, nikupate. 16 Nimepamba kitanda changu kwa matandiko, kwa vitu vyenye rangi mbalimbali, kitani cha Misri.+ 17 Nimetia kitanda changu manemane, udi na mdalasini.+ 18 Haya njoo, na tunywe na kushiba upendo mpaka asubuhi; na tufurahiane kwa maonyesho ya upendo.+ 19 Kwa maana mume hayumo nyumbani mwake; ameenda safari ya mbali.+ 20 Amechukua mfuko wa pesa mkononi mwake. Atarudi nyumbani kwake siku ya mwezi mpevu.”
21 Akampotosha kwa ushawishi wake mwingi.+ Akamtongoza kwa ulaini wa midomo yake.+ 22 Ghafula kijana huyo akamfuata,+ kama ng’ombe-dume anayeenda machinjoni, na kama mtu mpumbavu aliyefungwa pingu atiwe nidhamu, 23 mpaka mshale upasue ini lake,+ kama vile ndege anavyofanya haraka kuingia mtegoni,+ naye hajajua kwamba nafsi yake mwenyewe inahusika.+
24 Sasa basi, enyi wana, nisikilizeni na kutega sikio msikie maneno ya kinywa changu.+ 25 Moyo wako usikengeuke kuingia katika njia za mwanamke huyo. Usipotee na kuingia katika barabara zake.+ 26 Kwa maana amewafanya wengi waanguke wakiwa wamechinjwa,+ na wote ambao anawaua ni wengi.+ 27 Nyumba yake ni njia za kwenda katika Kaburi;*+ zinashuka kwenye vyumba vya ndani vya kifo.+