Methali
6 Mwanangu, ikiwa umekuwa mdhamini wa mwenzako,+ ikiwa wewe na mgeni mmepeana mikono katika mapatano,+ 2 ikiwa umenaswa na maneno ya kinywa chako,+ ikiwa umekamatwa na maneno ya kinywa chako, 3 basi chukua hatua hii, mwanangu, ujikomboe mwenyewe, kwa maana umejitia mkononi mwa mwenzako:+ Nenda ujinyenyekeze na kumsihi sana mwenzako.+ 4 Usiache macho yako yapate usingizi wowote, wala macho yako yenye kung’aa yasisinzie.+ 5 Jikomboe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji na kama ndege kutoka mkono wa mwindaji wa ndege.+
6 Mwendee chungu,+ ewe mvivu;+ zitazame njia zake upate kuwa na hekima. 7 Ijapokuwa hana kiongozi, ofisa wala mtawala, 8 yeye hutayarisha chakula chake wakati wa kiangazi;+ amekusanya akiba ya chakula chake wakati wa mavuno. 9 Ewe mvivu, utaendelea kulala hata wakati gani?+ Utaamka wakati gani kutoka katika usingizi wako?+ 10 Bado kulala kidogo, bado kusinzia kidogo, bado kukunja mikono ili kulala,+ 11 na hakika umaskini wako utakuja kama mnyang’anyi,+ na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.+
12 Mtu asiyefaa kitu,+ mtu wa mambo yenye kuumiza, anatembea akiwa na maneno mapotovu,+ 13 akikonyeza kwa jicho lake,+ akifanya ishara kwa mguu wake, na kuonyesha alama kwa vidole vyake.+ 14 Upotovu umo moyoni mwake.+ Anatunga jambo baya wakati wote.+ Huendelea kutokeza ugomvi.+ 15 Hiyo ndiyo sababu msiba wake utakuja ghafula;+ atavunjwa ghafula, wala hatapona.+
16 Kuna vitu sita ambavyo Yehova huchukia;+ naam, vitu saba vinachukiza nafsi yake:+ 17 macho ya majivuno,+ ulimi wa uwongo,+ na mikono inayomwaga damu isiyo na hatia,+ 18 moyo unaotunga hila zenye kuumiza,+ miguu iliyo myepesi kukimbilia ubaya,+ 19 shahidi wa uwongo anayesema uwongo,+ na yeyote anayetokeza magomvi kati ya ndugu.+
20 Ee mwanangu, shika amri ya baba yako,+ wala usiiache sheria ya mama yako.+ 21 Zifunge juu ya moyo wako sikuzote,+ zifunge shingoni pako.+ 22 Unapotembea huku na huku, itakuongoza;+ unapolala, itakulinda;+ na unapokuwa umeamka, hiyo yenyewe itakuhangaikia. 23 Kwa maana amri hiyo ni taa,+ na sheria ni nuru,+ nayo makaripio ya nidhamu ndiyo njia ya uzima,+ 24 yakulinde na mwanamke mbaya,+ na ulimi laini wa mwanamke mgeni.+ 25 Usiutamani urembo wake moyoni mwako,+ wala asikuchukue kwa macho yake yenye kung’aa,+ 26 kwa sababu ya mwanamke kahaba mtu hubaki tu na kipande cha mkate;+ lakini mke wa mwanamume mwingine, yeye huwinda hata nafsi yenye thamani.+ 27 Je, mtu anaweza kukusanya moto kifuani pake na mavazi yake yasiungue?+ 28 Au je, mtu anaweza kutembea juu ya makaa ya moto na miguu yake mwenyewe isiungue? 29 Ndivyo ilivyo kwa yule anayelala na mke wa mwenzake,+ mtu anayemgusa hatakosa kuadhibiwa.+ 30 Watu hawamdharau mwizi kwa sababu tu anaiba ili kushibisha nafsi yake akiwa na njaa. 31 Lakini, akipatikana, atalipa mara saba ya kiasi hicho; atatoa vitu vyote vyenye thamani vya nyumba yake.+ 32 Yeyote anayefanya uzinzi na mwanamke amepungukiwa moyoni;+ yule anayefanya hivyo anaiangamiza nafsi yake mwenyewe.+ 33 Atapata pigo na kukosa heshima,+ na shutuma yake haitafutiliwa mbali.+ 34 Kwa maana ghadhabu ya mwanamume ni wivu,+ naye hataonyesha huruma siku ya kulipiza kisasi.+ 35 Hatajali namna yoyote ya fidia, wala hataikubali zawadi yako hata iwe kubwa namna gani.