Methali
5 Mwanangu, sikiliza hekima yangu.+ Tega sikio usikie utambuzi wangu,+ 2 ili ulinde uwezo wako wa kufikiri;+ na midomo yako mwenyewe ilinde ujuzi.+
3 Kwa maana midomo ya mwanamke mgeni hudondoka-dondoka kama sega la asali,+ nalo kaakaa lake ni laini kuliko mafuta.+ 4 Lakini matokeo yake ni machungu kama pakanga;+ ni makali kama upanga wenye makali kuwili.+ 5 Miguu yake inashuka kwenye kifo.+ Hatua zake hushika Kaburi.*+ 6 Yeye hatafakari njia za uzima.+ Mapito yake yamepotoka wala hajui yanakoelekea.+ 7 Basi sasa, enyi wana, nisikilizeni+ wala msiache maneno ya kinywa changu.+ 8 Itenge njia yako mbali naye, wala usiukaribie mlango wa nyumba yake,+ 9 ili usije ukawapa wengine heshima yako,+ wala kukipa kilicho kikatili miaka yako;+ 10 ili wageni wasijishibishe kwa nguvu zako,+ wala vitu vyako ulivyovipata kwa maumivu visiwe ndani ya nyumba ya mgeni,+ 11 wala usije kulalamikia wakati wako ujao,+ nyama yako na mwili wako vitakapofikia mwisho.+ 12 Nawe utalazimika kusema: “Nimechukia nidhamu+ kama nini nao moyo wangu umedharau karipio+ kama nini! 13 Nami sikusikiliza sauti ya wafundishaji wangu,+ wala sikuwategea sikio langu walimu wangu.+ 14 Nimeingia kwa urahisi katika kila namna ya ubaya+ katikati ya kutaniko na kusanyiko.”+
15 Unywe maji ya birika lako mwenyewe, na maji yanayotiririka kutoka katikati ya kisima chako mwenyewe.+ 16 Je, chemchemi zako mwenyewe zitawanyike nje,+ na vijito vyako vya maji katika viwanja vya watu wote? 17 Na yawe yako peke yako, wala si ya wageni pamoja nawe.+ 18 Chemchemi yako ya maji na ibarikiwe,+ na ushangilie pamoja na mke wa ujana wako,+ 19 paa mwenye kupendeka na mbuzi wa milimani mwenye kuvutia.+ Na maziwa yake yakuleweshe nyakati zote.+ Upendo wake na ukufurahishe sikuzote.+ 20 Basi mwanangu, kwa nini umfurahie mwanamke mgeni au kukumbatia kifua cha mwanamke wa kigeni?+ 21 Kwa maana njia za mwanadamu ziko mbele za macho ya Yehova,+ naye anayatafakari mapito yake yote.+ 22 Makosa yake mwenyewe yatamkamata mwovu,+ naye atashikwa katika kamba za dhambi yake mwenyewe.+ 23 Atakufa yeye mwenyewe kwa sababu hakuna nidhamu,+ na kwa sababu ya upumbavu wake mwingi yeye hupotea.+