6 Wakati huo kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya,+ na ulimi wa bubu utapaaza sauti kwa furaha.+ Kwa maana maji yatakuwa yamebubujika katika nyika, na mito katika nchi tambarare ya jangwani.
13 Sasa walipoona maneno ya waziwazi ya Petro na Yohana, na kufahamu kwamba walikuwa watu wasio na elimu na wa kawaida tu,+ wakaanza kustaajabu. Nao wakaanza kutambua juu yao kwamba walikuwa pamoja na Yesu;+