Isaya
35 Nyika na nchi isiyo na maji itafurahi;+ na nchi tambarare ya jangwani itakuwa na shangwe na kuchanua maua kama zafarani.+ 2 Itachanua maua+ bila shaka, nayo itashangilia kwa shangwe na kwa kilio cha furaha.+ Itapewa utukufu wa Lebanoni,+ fahari ya Karmeli+ na ya Sharoni.+ Kutakuwa na wale watakaouona utukufu wa Yehova,+ fahari ya Mungu wetu.+
3 Tieni nguvu mikono iliyo dhaifu, na myaimarishe magoti yanayolegea-legea.+ 4 Waambieni wale wanaohangaika moyoni:+ “Iweni na nguvu.+ Msiogope.+ Tazameni! Mungu wenu atakuja na kisasi,+ Mungu akiwa na malipo.+ Yeye mwenyewe atakuja na kuwaokoa ninyi.”+
5 Wakati huo macho ya vipofu yatafunguliwa,+ na masikio ya viziwi yatazibuliwa.+ 6 Wakati huo kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya,+ na ulimi wa bubu utapaaza sauti kwa furaha.+ Kwa maana maji yatakuwa yamebubujika katika nyika, na mito katika nchi tambarare ya jangwani. 7 Na nchi iliyokaushwa na joto itakuwa kama dimbwi lenye matete, na nchi yenye kiu kama mabubujiko ya maji.+ Katika makao ya mbwa-mwitu,+ mahali pao pa kupumzika, patakuwa na majani mabichi na matete na mimea ya mafunjo.+
8 Na hakika kutakuwa na njia kuu hapo,+ ndiyo, njia; nayo itaitwa Njia ya Utakatifu.+ Asiye safi hatapita juu yake.+ Nayo itakuwa kwa ajili ya yule anayetembea katika njia hiyo, wala hakuna wapumbavu watakaotembea huku na huku juu yake. 9 Hakuna simba atakayekuwa hapo, na wanyama-mwitu wenye kunyafua hawatakuja juu yake.+ Hakuna yeyote atakayepatikana hapo;+ na waliokombolewa watatembea hapo.+ 10 Na wale hasa waliokombolewa na Yehova watarudi+ na kuja Sayuni kwa vigelegele vya shangwe;+ na kushangilia kutakuwa juu ya kichwa chao mpaka wakati usio na kipimo.+ Watafikia furaha na kushangilia, na huzuni na kuugua zitakimbia kabisa.+