16 Na kutakuwa na njia kuu+ kutoka Ashuru kwa ajili ya mabaki+ ya watu wake watakaobaki,+ kama ilivyokuwapo njia kwa ajili ya Israeli siku ile alipokuwa akiondoka katika nchi ya Misri.
10 Tokeni nje, tokeni nje kupitia malango. Fungueni njia ya watu.+ Fanyeni matuta, fanyeni matuta kwa ajili ya njia kuu. Ondoeni mawe juu yake.+ Inueni ishara kwa ajili ya vikundi vya watu.+
21 “Jisimamishie alama za barabara. Jiwekee vibao vya ishara.+ Kaza moyo wako juu ya njia kuu, njia ambayo utaiendea.+ Rudi, Ee bikira wa Israeli. Rudi kwenye haya majiji yako.+