3 Yeyote aliye katikati yenu ninyi watu wake wote, Mungu wake na awe pamoja naye.+ Basi na apande na kwenda Yerusalemu, huko Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli—yeye ndiye Mungu wa kweli+—iliyokuwa Yerusalemu.+
12 Naye hakika atainua ishara kwa ajili ya mataifa na kukusanya watu wa Israeli waliotawanywa;+ na watu wa Yuda waliotawanywa atawakusanya pamoja kutoka miisho minne ya dunia.+
3 Enyi wakaaji wote wa nchi yenye kuzaa+ nanyi wakaaji wa dunia, mtaona maono kama wakati ishara inapoinuliwa juu ya milima,+ nanyi mtasikia sauti kama wakati baragumu inapopigwa.+
22 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama! Nitayainulia mataifa mkono wangu,+ nami nitaviinulia vikundi vya watu ishara yangu.+ Nao wataleta watoto wako katika kifua, nao watawabeba binti zako juu ya bega.+