Isaya
18 Lo, nchi ya wadudu wenye kuvuma walio na mabawa, iliyoko katika eneo la mito ya Ethiopia!+ 2 Hiyo ndiyo inayotuma wajumbe+ kwa njia ya bahari, na kwa njia ya vyombo vya mafunjo juu ya uso wa maji, ikisema: “Nendeni, enyi wajumbe wepesi, kwa taifa lenye watu warefu na walio laini, kwa watu wenye kuogopesha kila mahali, taifa lenye nguvu zinazodumu na lenye kukanyaga-kanyaga, ambalo mito imeifagilia mbali nchi yake.”+
3 Enyi wakaaji wote wa nchi yenye kuzaa+ nanyi wakaaji wa dunia, mtaona maono kama wakati ishara inapoinuliwa juu ya milima,+ nanyi mtasikia sauti kama wakati baragumu inapopigwa.+ 4 Kwa maana Yehova ameniambia hivi: “Nitakaa bila usumbufu na kupatazama mahali pangu palipofanywa imara,+ kama joto linalometameta pamoja na nuru,+ kama wingu la umande katika joto la mavuno.+ 5 Kwa maana kabla ya mavuno, wakati ua linapofikia ukamilifu na ua linapokuwa zabibu inayoiva, lazima mtu pia akate vitawi kwa miundu na kuviondoa vikonyo, lazima avikate.+ 6 Wote pamoja wataachiwa ndege mwenye kuwinda wa milimani na mnyama wa dunia.+ Na juu yao ndege mwenye kuwinda atakaa wakati wa kiangazi, na juu yao kila mnyama wa dunia atakaa wakati wa mavuno.+
7 “Katika wakati huo zawadi italetwa kwa Yehova wa majeshi,+ kutoka kwa watu warefu na walio laini,+ kutoka kwa watu wenye kuogopesha kila mahali, taifa lenye nguvu zinazodumu na lenye kukanyaga-kanyaga, ambalo mito imeifagilia mbali nchi yake, kwenye mahali pa jina la Yehova wa majeshi, Mlima Sayuni.”+