12 Nami nitapita katikati ya nchi ya Misri usiku huu+ na kumpiga kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri, kuanzia mwanadamu hata mnyama;+ nami nitatekeleza hukumu+ juu ya miungu yote ya Misri. Mimi ni Yehova.+
12 Nami nitawasha moto katika nyumba za miungu ya Misri;+ naye hakika ataiteketeza na kuipeleka mateka na kujifunga yeye mwenyewe katika nchi ya Misri, kama mchungaji anavyojifunga katika vazi lake,+ na kwa kweli ataondoka huko kwa amani.
25 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema, ‘Tazama, ninakaza fikira zangu juu ya Amoni+ kutoka No+ na juu ya Farao na juu ya Misri na juu ya miungu+ yake na juu ya wafalme+ wake, juu ya Farao na juu ya wale wote wanaomtegemea.’+
13 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Nitaangamiza pia sanamu za mavi+ na kufanya miungu isiyo na thamani ikome katika Nofu,+ na hakutakuwa tena na mkuu kutoka katika nchi ya Misri; nami hakika nitatia hofu katika nchi ya Misri.+