8 Na watu wamekuwa na wasiwasi.+ Utungu na uchungu wa kuzaa zimewashika; wana uchungu kama mwanamke anayezaa.+ Wanatazamana kwa mshangao. Nyuso zao ni nyuso zilizowaka.+
3 Ndiyo sababu viuno vyangu vimejaa maumivu makali.+ Utungu umenishika, kama utungu wa mwanamke anayezaa.+ Nimevurugika hivi kwamba sisikii; nimeingiwa na wasiwasi hivi kwamba sioni.
22 Tazama! Mtu atapaa na kurukia mawindo kama tai,+ naye atanyoosha mabawa yake juu ya Bosra;+ na moyo wa wanaume wenye nguvu wa Edomu siku hiyo utakuwa kama moyo wa mke aliye na taabu ya kuzaa mtoto.”+
9 “Basi ni kwa nini unaendelea kupiga kelele?+ Je, hamna mfalme ndani yako, au je, mshauri wako mwenyewe ameangamizwa, hata maumivu kama yale ya mwanamke anayezaa yakakushika?+
3 Wakati watakapokuwa wakisema:+ “Amani+ na usalama!” ndipo uharibifu+ wa ghafula utakapokuwa juu yao mara moja kama vile maumivu ya taabu juu ya mwanamke mwenye mimba;+ nao hawataponyoka hata kidogo.+