27 “ ‘Na ufalme na utawala na ukuu wa falme zote chini ya mbingu zote wakapewa watu ambao ni watakatifu wa Aliye Mkuu Zaidi.+ Ufalme wao ni ufalme unaodumu mpaka wakati usio na kipimo,+ na tawala zote zitawatumikia na kuwatii wao.’+
28 Kwa hiyo, kwa kuwa tutapokea ufalme ambao hauwezi kutikiswa,+ acheni tuendelee kuwa na fadhili zisizostahiliwa, ambazo kupitia hizo tunaweza kumtolea Mungu kwa njia inayokubalika utumishi mtakatifu kwa woga wa kimungu na heshima.+
5 Sikilizeni, ndugu zangu wapendwa. Mungu alichagua walio maskini+ kwa habari ya ulimwengu ili wawe matajiri+ katika imani na warithi wa ufalme, aliowaahidi wale wanaompenda,+ sivyo?