Mathayo 27:24 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 24 Alipoona kwamba haikufaidi kitu bali, badala yake, ghasia zilikuwa zikitokea, Pilato alichukua maji+ na kunawa mikono yake mbele ya ule umati, akisema: “Mimi sina hatia ya damu ya mtu huyu. Shauri yenu.” Luka 23:4 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 4 Ndipo Pilato akawaambia wakuu wa makuhani na ule umati: “Mimi sioni uhalifu wa mtu huyu.”+ Yohana 15:25 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 25 Lakini ni ili neno lililoandikwa katika Sheria yao lipate kutimizwa, ‘Walinichukia bila sababu.’+
24 Alipoona kwamba haikufaidi kitu bali, badala yake, ghasia zilikuwa zikitokea, Pilato alichukua maji+ na kunawa mikono yake mbele ya ule umati, akisema: “Mimi sina hatia ya damu ya mtu huyu. Shauri yenu.”