19 Kwa hiyo, Yesu akajibu, akawaambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mwana hawezi kufanya hata jambo moja kwa uamuzi wake mwenyewe, ila tu lile analomwona Baba akifanya.+ Kwa maana mambo yoyote yale ambayo Yule hufanya, mambo hayo Mwana pia hufanya vivyo hivyo.