4 Kaeni katika muungano pamoja nami, na mimi katika muungano pamoja nanyi.+ Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa matunda likiwa peke yake lisipokaa katika mzabibu, vivyo hivyo ninyi hamwezi, msipokaa katika muungano pamoja nami.+
5 Mimi ndiye mzabibu, ninyi ndio matawi. Yule ambaye hukaa katika muungano pamoja nami, na mimi katika muungano pamoja naye, huyo huzaa matunda mengi;+ kwa sababu bila mimi hamwezi kufanya lolote kamwe.