Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 21:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Lakini Sara alikuwa akiona kwamba mwana ambaye Hagari+ Mmisri alimzalia Abrahamu, alikuwa akimdhihaki Isaka.+

  • Kutoka 1:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kwa hiyo, Wamisri wakawalazimisha Waisraeli kuwa watumwa na kuwatesa kikatili.+ 14 Wakafanya maisha yao yawe machungu kwa kazi ngumu ya kutengeneza saruji ya udongo wa mfinyanzi na matofali na katika kila aina ya utumwa shambani. Naam, waliwalazimisha wafanye kazi ngumu chini ya hali ngumu sana katika kila aina ya utumwa.+

  • Kutoka 3:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kisha Yehova akasema: “Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walio Misri, nami nimesikia kilio chao kwa sababu ya wale wanaowalazimisha kufanya kazi; ninajua vema maumivu yao.+

  • Matendo 7:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Isitoshe, Mungu alimwambia kwamba wazao* wake wangekuwa wageni katika nchi ambayo si yao na kwamba watu wa nchi hiyo wangewafanya kuwa watumwa na kuwatesa* kwa miaka 400.+ 7 ‘Nami nitalihukumu taifa hilo ambalo watalitumikia,’+ Mungu akasema, ‘na baada ya mambo hayo watatoka na kunitolea utumishi mtakatifu mahali hapa.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki