-
Kutoka 1:13, 14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Kwa hiyo, Wamisri wakawalazimisha Waisraeli kuwa watumwa na kuwatesa kikatili.+ 14 Wakafanya maisha yao yawe machungu kwa kazi ngumu ya kutengeneza saruji ya udongo wa mfinyanzi na matofali na katika kila aina ya utumwa shambani. Naam, waliwalazimisha wafanye kazi ngumu chini ya hali ngumu sana katika kila aina ya utumwa.+
-
-
Matendo 7:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Isitoshe, Mungu alimwambia kwamba wazao* wake wangekuwa wageni katika nchi ambayo si yao na kwamba watu wa nchi hiyo wangewafanya kuwa watumwa na kuwatesa* kwa miaka 400.+ 7 ‘Nami nitalihukumu taifa hilo ambalo watalitumikia,’+ Mungu akasema, ‘na baada ya mambo hayo watatoka na kunitolea utumishi mtakatifu mahali hapa.’+
-