Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 7:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Yehova anasema hivi: “Kwa jambo hili utajua kwamba mimi ni Yehova.+ Tazama ninayapiga maji ya Mto Nile kwa fimbo hii iliyo mkononi mwangu, nayo yatabadilika na kuwa damu.

  • Kutoka 8:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Kisha Musa akamwambia Farao: “Kwa heshima yako niambie wakati unaotaka nimwombe Mungu awaondoe vyura kutoka kwako, kutoka kwa watumishi wako, kutoka kwa watu wako, na kutoka katika nyumba zenu. Watabaki katika Mto Nile tu.” 10 Farao akamwambia: “Kesho.” Basi Musa akasema: “Itakuwa kama unavyosema, ili ujue kwamba hakuna yeyote aliye kama Yehova Mungu wetu.+

  • Kutoka 8:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Siku hiyo, hakika nitaitenga nchi ya Gosheni, wanakoishi watu wangu. Hakuna nzi yeyote atakayepatikana huko,+ na kwa jambo hilo utajua kwamba mimi, Yehova, niko humu nchini.+

  • Kutoka 9:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Kwa hiyo Musa akamwambia: “Mara tu nitakapoondoka jijini, nitainyoosha mikono yangu mbele za Yehova. Ngurumo itakoma na mvua ya mawe haitaendelea kunyesha, ili ujue kwamba dunia ni ya Yehova.+

  • Kutoka 14:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Nitauacha moyo wa Farao uwe mkaidi,+ naye atawafuatia, nami nitajipatia utukufu kupitia Farao na jeshi lake lote;+ na Wamisri watajua kwa hakika kwamba mimi ni Yehova.”+ Basi Waisraeli wakafanya hivyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki