Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 9:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kwa maana sasa ninayaelekeza mapigo yangu yote niupige moyo wako, niwapige watumishi wako, na watu wako, ili ujue kwamba hakuna yeyote aliye kama mimi katika dunia yote.+

  • Kutoka 15:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Ni nani kati ya miungu aliye kama wewe, Ee Yehova?+

      Ni nani aliye kama wewe, unayejidhihirisha mwenyewe kuwa mkuu katika utakatifu?+

      Wewe unayestahili kuogopwa kwa nyimbo za sifa, Wewe unayetenda mambo yanayostaajabisha.+

  • Zaburi 83:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Na watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova,+

      Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.+

  • Zaburi 86:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Hakuna yeyote aliye kama wewe kati ya miungu, Ee Yehova,+

      Hakuna kazi zilizo kama kazi zako.+

  • Isaya 46:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  9 Kumbukeni mambo ya kwanza* ya zamani za kale,

      Kwamba mimi ni Mungu, na hakuna mwingine.

      Mimi ni Mungu, na hakuna aliye kama mimi.+

  • Yeremia 10:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Hakuna yeyote aliye kama wewe, Ee Yehova.+

      Wewe ni mkuu, na jina lako ni kuu na lenye nguvu.

       7 Ni nani asiyepaswa kukuogopa, Ee Mfalme wa mataifa,+ kwa maana ni jambo linalofaa;

      Kwa sababu kati ya watu wote wenye hekima wa mataifa na kati ya falme zao zote,

      Hakuna yeyote yule aliye kama wewe.+

  • Waroma 9:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kwa maana andiko linamwambia Farao: “Kwa sababu hii nimekuacha ubaki: ili nionyeshe nguvu zangu kuhusiana na wewe na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki