Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 9:15, 16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Kwa maana kufikia sasa ningekuwa nimeunyoosha mkono wangu kwa nguvu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo kali sana, nawe ungekuwa umefutiliwa* mbali kutoka duniani. 16 Lakini nimekuacha uendelee kuishi kwa sababu hii hasa: ili nikuonyeshe nguvu zangu na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.+

  • Kutoka 15:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Ni nani kati ya miungu aliye kama wewe, Ee Yehova?+

      Ni nani aliye kama wewe, unayejidhihirisha mwenyewe kuwa mkuu katika utakatifu?+

      Wewe unayestahili kuogopwa kwa nyimbo za sifa, Wewe unayetenda mambo yanayostaajabisha.+

  • Kutoka 18:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kisha Yethro akasema: “Yehova na asifiwe, aliyekuokoa kutoka Misri na kutoka kwa Farao, na kuwaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wamisri. 11 Sasa ninajua kwamba Yehova ni mkuu kuliko miungu mingine yote,+ kwa sababu ya mambo aliyowafanyia wale waliowatendea watu wake kwa kiburi.”

  • Yoshua 2:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Akawaambia: “Najua kwamba Yehova atawapa nchi hii+ na tumeshikwa na hofu kwa sababu yenu.+ Wakaaji wote wa nchi wamevunjika moyo kwa sababu yenu,+ 10 kwa maana tumesikia jinsi Yehova alivyoyakausha maji ya Bahari Nyekundu* mbele yenu mlipotoka Misri+ na mambo mliyowatendea wale wafalme wawili wa Waamori, yaani, Sihoni+ na Ogu,+ waliokuwa ng’ambo ya* Yordani, mliowaangamiza kabisa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki