-
Kutoka 9:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Kwa maana kufikia sasa ningekuwa nimeunyoosha mkono wangu kwa nguvu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo kali sana, nawe ungekuwa umefutiliwa* mbali kutoka duniani. 16 Lakini nimekuacha uendelee kuishi kwa sababu hii hasa: ili nikuonyeshe nguvu zangu na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.+
-
-
Yoshua 2:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Akawaambia: “Najua kwamba Yehova atawapa nchi hii+ na tumeshikwa na hofu kwa sababu yenu.+ Wakaaji wote wa nchi wamevunjika moyo kwa sababu yenu,+ 10 kwa maana tumesikia jinsi Yehova alivyoyakausha maji ya Bahari Nyekundu* mbele yenu mlipotoka Misri+ na mambo mliyowatendea wale wafalme wawili wa Waamori, yaani, Sihoni+ na Ogu,+ waliokuwa ng’ambo ya* Yordani, mliowaangamiza kabisa.
-