Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 8:21, 22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Lakini usipowaruhusu watu wangu waende zao, nitakuletea nzi,* wewe, watumishi wako, na watu wako, nao wataingia katika nyumba zako; na nyumba za Misri zitajaa nzi hao, nao wataifunika hata ardhi ambayo Wamisri wamesimama juu yake. 22 Siku hiyo, hakika nitaitenga nchi ya Gosheni, wanakoishi watu wangu. Hakuna nzi yeyote atakayepatikana huko,+ na kwa jambo hilo utajua kwamba mimi, Yehova, niko humu nchini.+

  • Kutoka 9:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 tazama! mkono wangu mimi Yehova+ utaipiga mifugo yenu iliyo shambani. Nitawaletea pigo kali sana farasi, punda, ngamia, ng’ombe, na makundi yenu.+

  • Kutoka 9:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Na kesho yake Yehova akafanya hivyo, kila aina ya mifugo ya Wamisri ikaanza kufa,+ lakini hakuna mnyama hata mmoja wa Waisraeli aliyekufa.

  • Kutoka 9:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Ila tu mvua hiyo ya mawe haikunyesha katika nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.+

  • Kutoka 11:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Lakini hakuna hata mbwa atakayewabwekea* Waisraeli, iwe ni wanadamu au mifugo yao, ili mjue kwamba mimi Yehova ninaweza kutofautisha kati ya Wamisri na Waisraeli.’+

  • Kutoka 12:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Ile damu itakuwa ishara inayoonyesha nyumba mtakazokuwamo; nami nitaiona damu hiyo na kupita juu yenu, na pigo halitawajia na kuwaangamiza ninyi nitakapoipiga nchi ya Misri.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki