-
Kutoka 10:8-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Kwa hiyo Musa na Haruni wakarudishwa kwa Farao, akawaambia: “Nendeni, mkamtumikie Yehova Mungu wenu. Lakini ni nani hasa watakaoenda?” 9 Musa akamjibu: “Tutaenda na vijana wetu, wazee wetu, wana wetu, mabinti wetu, kondoo wetu, na ng’ombe wetu,+ kwa maana tutamfanyia Yehova sherehe.”+ 10 Akawaambia: “Ikiwa nitawaruhusu ninyi na watoto wenu mwende, basi kwa kweli Yehova yuko pamoja nanyi!+ Ni wazi kwamba mnakusudia kutenda jambo fulani ovu. 11 Hapana! Ni wanaume wenu peke yao watakaoenda kumtumikia Yehova, kwa sababu hilo ndilo mliloomba.” Basi wakafukuzwa kutoka mbele ya Farao.
-