-
Hesabu 16:39, 40Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
39 Basi kuhani Eleazari akachukua vyetezo vya shaba vilivyoletwa na wale wanaume waliokuwa wameteketezwa, akavipiga na kuvinyoosha ili vifunike madhabahu, 40 kama Yehova alivyomwambia kupitia Musa. Viliwakumbusha Waisraeli kwamba mtu yeyote asiye na idhini* ambaye si mzao wa Haruni hapaswi kukaribia madhabahu ili kumfukizia Yehova+ uvumba na kwamba mtu yeyote asiwe kama Kora na wale waliomuunga mkono.+
-
-
1 Samweli 2:27, 28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
27 Mtu wa Mungu alimjia Eli na kumwambia, “Yehova anasema hivi: ‘Je, sikujitambulisha waziwazi kwa watu wa nyumba ya baba yako walipokuwa Misri wakiwa watumwa wa nyumba ya Farao?+ 28 Naye alichaguliwa kutoka katika makabila yote ya Israeli+ ili anitumikie akiwa kuhani wangu na kupanda juu ya madhabahu yangu+ kutoa dhabihu, kufukiza uvumba,* na kuvaa efodi mbele zangu; nami niliwapa watu wa nyumba ya babu yako dhabihu zote zinazochomwa kwa moto zilizotolewa na Waisraeli.*+
-