-
Kutoka 29:38-42Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
38 “Hivi ndivyo vitu utakavyotoa kwenye madhabahu: kila siku, kwa kuendelea,+ utatoa wanakondoo dume wawili wenye umri wa mwaka mmoja. 39 Mtoe mwanakondoo dume mmoja asubuhi na yule mwingine jioni kabla ya giza kuingia.*+ 40 Sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja* ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini* ya mafuta ya zeituni zilizopondwa, na toleo la kinywaji la robo ya hini ya divai, vitatolewa pamoja na mwanakondoo dume wa kwanza. 41 Utamtoa mwanakondoo dume wa pili jioni kabla ya giza kuingia,* pamoja na matoleo ya nafaka na kinywaji kama yale ya asubuhi. Utamtoa akiwa harufu inayopendeza,* dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto. 42 Itakuwa dhabihu ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ukawaida katika vizazi vyenu vyote kwenye mlango wa hema la mkutano mbele za Yehova, mahali ambapo nitawatokea ili kuzungumza nanyi.+
-