-
Mambo ya Walawi 21:21, 22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Mtu yeyote wa uzao wa* kuhani Haruni ambaye ana kasoro hatakaribia mahali patakatifu ili kutoa dhabihu za Yehova zinazochomwa kwa moto. Kwa sababu ana kasoro, hapaswi kupakaribia ili kutoa mkate wa Mungu wake. 22 Anaweza kula mkate wa Mungu wake kutoka kati ya vitu vitakatifu kabisa+ na kutoka kati ya vitu vitakatifu.+
-