Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 2:3-7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Chochote kinachobaki cha toleo hilo la nafaka kitakuwa cha Haruni na wanawe,+ kitakuwa kitu kitakatifu kabisa+ kutoka kwa dhabihu za Yehova zinazochomwa kwa moto.

      4 “‘Mkitoa nafaka ambayo imeokwa kwenye jiko, inapaswa kuwa ya unga laini, mikate ya mviringo isiyo na chachu na iliyokandwa kwa mafuta, au mikate myembamba isiyo na chachu ambayo imepakwa mafuta.+

      5 “‘Mkitoa toleo la nafaka kutoka katika kiokeo,+ inapaswa kuwa ya unga laini usio na chachu, uliokandwa kwa mafuta. 6 Toleo hilo litavunjwa vipandevipande na mafuta yatamiminwa juu yake.+ Ni toleo la nafaka.

      7 “‘Mkitoa toleo la nafaka iliyokaangwa kwenye kikaangio, linapaswa kuwa la unga laini uliokandwa kwa mafuta.

  • Hesabu 18:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Hivi ndivyo vitakavyokuwa vitu vyenu kutoka katika matoleo yote matakatifu kabisa yanayochomwa kwa moto: matoleo yao yote, kutia ndani matoleo yao ya nafaka+ na dhabihu zao za dhambi+ na dhabihu zao za hatia+ wanazoniletea. Ni vitu vitakatifu kabisa kwako na wanao.

  • 1 Wakorintho 9:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Je, hamjui kwamba watu wanaofanya kazi takatifu hula vitu vya hekalu, na kwamba wale wanaohudumu kwa kawaida kwenye madhabahu hupata fungu lao kutoka kwenye madhabahu?+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki