Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 29:27, 28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Utakitakasa kidari cha toleo la kutikiswa na ule mguu wa fungu takatifu ambao ulitikiswa na ambao ulichukuliwa kutoka kwa yule kondoo dume wa kumweka rasmi kuhani,+ aliyetolewa kwa ajili ya Haruni na wanawe. 28 Vitu hivyo vitakuwa vya Haruni na wanawe kulingana na sheria ya kudumu itakayotekelezwa na Waisraeli, kwa sababu vitu hivyo ni fungu takatifu, navyo vitakuwa fungu takatifu litakalotolewa na Waisraeli.+ Ni fungu lao takatifu kwa Yehova kutoka katika dhabihu zao za ushirika.+

  • Mambo ya Walawi 10:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Pia, wewe na wanao na binti zako+ mtakula kidari cha toleo la kutikiswa na mguu wa fungu takatifu+ mkiwa mahali safi kwa sababu vitu hivyo vimetolewa ili kuwa posho yako na posho ya wanao kutoka kwenye dhabihu za ushirika za Waisraeli.

  • Hesabu 6:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Halafu kuhani atavitikisa vitu hivyo kwenda mbele na nyuma vikiwa toleo la kutikiswa mbele za Yehova.+ Ni vitu vitakatifu kwa kuhani, pamoja na kidari cha toleo la kutikiswa na mguu uliotolewa kama mchango.+ Baada ya hayo, Mnadhiri huyo anaweza kunywa divai.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki