Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 29:26-28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “Halafu chukua kidari cha kondoo dume wa kumweka rasmi kuhani,+ anayetolewa kwa ajili ya Haruni, nawe ukitikise kwenda mbele na nyuma kikiwa toleo la kutikiswa mbele za Yehova, nacho kitakuwa fungu lako. 27 Utakitakasa kidari cha toleo la kutikiswa na ule mguu wa fungu takatifu ambao ulitikiswa na ambao ulichukuliwa kutoka kwa yule kondoo dume wa kumweka rasmi kuhani,+ aliyetolewa kwa ajili ya Haruni na wanawe. 28 Vitu hivyo vitakuwa vya Haruni na wanawe kulingana na sheria ya kudumu itakayotekelezwa na Waisraeli, kwa sababu vitu hivyo ni fungu takatifu, navyo vitakuwa fungu takatifu litakalotolewa na Waisraeli.+ Ni fungu lao takatifu kwa Yehova kutoka katika dhabihu zao za ushirika.+

  • Mambo ya Walawi 7:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Kuhani atayateketeza mafuta hayo kwenye madhabahu ili yafuke moshi,+ lakini kidari kitakuwa cha Haruni na wanawe.+

  • Mambo ya Walawi 7:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Kwa maana nachukua kidari cha toleo la kutikiswa na mguu wa lile fungu takatifu kutoka kwa dhabihu za ushirika za Waisraeli na kumpa kuhani Haruni na wanawe. Ni sheria ya kudumu kwa Waisraeli.+

  • Mambo ya Walawi 9:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Hata hivyo, Haruni akatikisa vidari na mguu wa kulia kwenda mbele na nyuma kuwa toleo la kutikiswa mbele za Yehova, kama Musa alivyoamuru.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki