-
Kutoka 29:26-28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
26 “Halafu chukua kidari cha kondoo dume wa kumweka rasmi kuhani,+ anayetolewa kwa ajili ya Haruni, nawe ukitikise kwenda mbele na nyuma kikiwa toleo la kutikiswa mbele za Yehova, nacho kitakuwa fungu lako. 27 Utakitakasa kidari cha toleo la kutikiswa na ule mguu wa fungu takatifu ambao ulitikiswa na ambao ulichukuliwa kutoka kwa yule kondoo dume wa kumweka rasmi kuhani,+ aliyetolewa kwa ajili ya Haruni na wanawe. 28 Vitu hivyo vitakuwa vya Haruni na wanawe kulingana na sheria ya kudumu itakayotekelezwa na Waisraeli, kwa sababu vitu hivyo ni fungu takatifu, navyo vitakuwa fungu takatifu litakalotolewa na Waisraeli.+ Ni fungu lao takatifu kwa Yehova kutoka katika dhabihu zao za ushirika.+
-