Mwanzo 17:12 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 12 Katika vizazi vyenu vyote, kila mwanamume miongoni mwenu mwenye umri wa siku nane ni lazima atahiriwe,+ yeyote anayezaliwa nyumbani mwenu na yeyote ambaye si mmoja wa uzao wenu* na yeyote aliyenunuliwa kwa pesa kutoka kwa mgeni. Mwanzo 21:4 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 4 Na Abrahamu akamtahiri Isaka mwanawe akiwa na umri wa siku nane, kama Mungu alivyokuwa amemwamuru.+ Luka 1:59 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 59 Siku ya nane wakaja kumtahiri huyo mtoto,+ nao walitaka kumpa jina la baba yake, Zekaria. Luka 2:21, 22 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 21 Baada ya siku nane, wakati ulipofika wa kumtahiri,+ wakampa jina Yesu, jina alilopewa na malaika kabla ya Maria kupata mimba.+ 22 Pia, wakati ulipofika wa kuwatakasa kulingana na Sheria ya Musa,+ wakamleta Yerusalemu ili kumtoa kwa Yehova,* Yohana 7:22 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 22 Kwa hiyo Musa aliwapa tohara+—si kwamba inatoka kwa Musa, bali inatoka kwa mababu+—nanyi mnamtahiri mtu siku ya sabato.
12 Katika vizazi vyenu vyote, kila mwanamume miongoni mwenu mwenye umri wa siku nane ni lazima atahiriwe,+ yeyote anayezaliwa nyumbani mwenu na yeyote ambaye si mmoja wa uzao wenu* na yeyote aliyenunuliwa kwa pesa kutoka kwa mgeni.
4 Na Abrahamu akamtahiri Isaka mwanawe akiwa na umri wa siku nane, kama Mungu alivyokuwa amemwamuru.+
21 Baada ya siku nane, wakati ulipofika wa kumtahiri,+ wakampa jina Yesu, jina alilopewa na malaika kabla ya Maria kupata mimba.+ 22 Pia, wakati ulipofika wa kuwatakasa kulingana na Sheria ya Musa,+ wakamleta Yerusalemu ili kumtoa kwa Yehova,*
22 Kwa hiyo Musa aliwapa tohara+—si kwamba inatoka kwa Musa, bali inatoka kwa mababu+—nanyi mnamtahiri mtu siku ya sabato.