9 Lakini tunamwona Yesu, aliyefanywa kuwa mdogo kidogo kuliko malaika,+ sasa amevikwa taji la utukufu na heshima kwa kupatwa na kifo,+ ili kwa fadhili zisizostahiliwa za Mungu aonje kifo kwa ajili ya kila mtu.+
27 Tofauti na makuhani hao wakuu, hahitaji kutoa dhabihu kila siku,+ kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe kisha kwa ajili ya dhambi za watu,+ kwa sababu alifanya hivyo mara moja kwa wakati wote alipojitoa mwenyewe.+
7 lakini kuhani mkuu huingia ndani ya chumba cha pili akiwa peke yake mara moja kwa mwaka,+ akiwa na damu,+ ambayo huitoa kwa ajili yake mwenyewe+ na kwa ajili ya dhambi ambazo watu+ walifanya bila kujua.
12 Aliingia mahali patakatifu, si kwa damu ya mbuzi na ya ng’ombe dume wachanga, bali kwa damu yake mwenyewe,+ mara moja kwa wakati wote, na kupata ukombozi wa* milele kwa ajili yetu.+