Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 20:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 “‘Kwa hakika nitamkataa na kumwangamiza mtu yeyote anayetafuta ushauri kutoka kwa watu wanaowasiliana na roho+ na pia wabashiri+ ili kufanya ukahaba wa kiroho pamoja nao.+

  • Kumbukumbu la Torati 18:10-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Asipatikane miongoni mwenu mtu yeyote anayemteketeza* motoni+ mwanawe au binti yake, mtu yeyote anayefanya uaguzi,*+ mtu yeyote anayefanya uchawi,+ mtu yeyote anayetafuta ishara za ubashiri,+ mlozi,+ 11 mtu yeyote anayewafunga wenzake kwa uchawi, mtu yeyote anayetafuta ushauri kutoka kwa watu wanaowasiliana na roho,+ mpiga ramli,+ au mtu yeyote anayetafuta habari kuhusu wafu.+ 12 Kwa maana mtu yeyote anayefanya mambo haya ni chukizo kwa Yehova, na kwa sababu ya mazoea haya yanayochukiza, Yehova Mungu wenu anayafukuza mataifa hayo kutoka mbele yenu.

  • 1 Mambo ya Nyakati 10:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kwa hiyo Sauli alikufa kwa sababu hakuwa mwaminifu kwa Yehova kwa maana hakutii neno la Yehova,+ na pia kwa sababu alitafuta ushauri kutoka kwa mtu aliyewasiliana na roho+

  • Isaya 8:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Nao wakiwaambia: “Tafuteni habari kutoka kwa wale wanaowasiliana na roho au wabashiri wanaonong’oneza na kutoa sauti za chini,” je, watu hawapaswi kutafuta habari kutoka kwa Mungu wao? Je, wanapaswa kutafuta habari kutoka kwa wafu kwa ajili ya walio hai?+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki